Kukokana na kuzamia nchini paris kwa muda wa miaka 26 Luciana Demingongo sasa ameamua kutoa album yake ya nne ambapo ni album ambayo ipo nje ya band yake ambayo anaitumikia kwa sasa ya zimpompa pompa band
Demingongo ambae amewahi kuimba band mbalimbali nchini Congo ambapo aneimba na moja ya wanamuziki kama vile Awilo Longomba ambapo kipindi hicho alikuwa ni mpiga gitaa yeye akiwa muimbaji walifanya kazi nyingi sana mpaka awilo kuhamia uimbaji
Demigongo amesema hivi karibuni anatarajia kuja DRC kusalimia na ameweza kutaja album ambazo anazo mpaka sasa ambapo album yake ya kwanza aliitoa mwaka 2012 iliyofahamika kama DEMINGONGO ZANZIBAR ambayo inanyimbo 9 moja wapo ni,Tempo,resistance,Rokia,Chanteau Rouge,Ange Volcan,Adisha,Zanzibar na Et poutant
A lbum yake ya pili inafahamika kama LUCIANA DEMINGONGO ANGE VOLICAN na album yake ya tatu inafahamika kama LUCIANA DEMINGONGO ROKIA.
Demingongo amesema album yake ya nne ni album ambayo itakuwa ya kuotea mbali zaidi kwani amejipanga zaidi na ameifanya kwa umakini wa hali ya juu za na hivyo amewaomba mashabiki wote wote wa muziki wa dance Congo na Tanzania kusikiliza nyimbo mbalimbali ili kupata jumbe ambazo zinapatikana katika nyimbo hizo
AFRIQUE MOTO PAMOJA
Namkubali sana huyo jamaa
ReplyDeleteGood music that's need to be given enough airplay, fantastic album
ReplyDelete